Kifo cha Yesu
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kifo cha Yesu msalabani kilitokea huko Yerusalemu, nchini Israeli, siku ya Ijumaa, labda tarehe 7 Aprili 30 BK[1][2].
Maelezo zaidi Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu, Mazingira ya Yesu ...
Funga
Tukio hilo[3], pamoja na ufufuko wa Yesu unaosadikiwa na Ukristo kutokea siku ya tatu (Jumapili ya Pasaka), ndiyo kiini cha imani ya dini hiyo mpya iliyotokana na ile ya Uyahudi.
Kwa Wakristo fumbo hilo la Pasaka ndilo kilele cha historia ya wokovu inayotangazwa na Biblia ya Kikristo.
Fumbo hilo lilisababisha kazi nyingi za sanaa ya Kikristo, hasa uchoraji na uchongaji.