Miujiza ya Yesu
From Wikipedia, the free encyclopedia
Miujiza ya Yesu ni matendo yapitayo sheria za maumbile[1] yaliyofanywa na Yesu kadiri yanavyosema maandiko matakatifu ya Ukristo na Uislamu. Ilikuwa mingi sana; hata hivyo Injili ya Yohane (21:25) inashuhudia kwamba michache tu imeandikwa.[2][3][4]
Maelezo zaidi Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu, Mazingira ya Yesu ...
Funga
Kati ya miujiza hiyo, kuna mazinguo ya kufukuza pepo wachafu, uponyaji wa maradhi mbalimbali (homa, ukoma, safura, kupooza mkono au mwili mzima, kupinda kwa mgongo, kutokwa damu mfululizo, upofu, uziwi, ububu na vilema vingine), ufufuo wa wafu, na ushindi juu ya uasilia (kama kugeuza maji kuwa divai, kutembea juu ya maji ya ziwa, kutuliza dhoruba na kuzidisha mkate na kitoweo cha samaki).[5][6]