Familia takatifu
From Wikipedia, the free encyclopedia
Familia takatifu katika Ukristo ni hasa ile iliyoundwa na Mtoto Yesu, Bikira Maria na mtakatifu Yosefu.
Maelezo zaidi Mfululizo wa kurasa juu ya Yesu, Mazingira ya Yesu ...
Funga
Kwa imani ya Wakristo ni kwamba Mungu alipomtuma Mwanae pekee kujifanya mtu hakutaka azaliwe nje ya familia, kwa kuwa hiyo ndiyo mpango wake asili kwa ajili ya watu tangu alipoumba Adamu na Eva akawabariki wazaliane.
Heshima kwa Familia takatifu katika Kanisa Katoliki ilianzishwa rasmi na Fransisko wa Laval, askofu wa kwanza wa New France (Kanada) katika karne ya 17.