Macau
From Wikipedia, the free encyclopedia
Macau (Kireno: Macau; Kichina: 澳門; pinyin: Àomén), rasmi Mkoa Maalum wa Utawala wa Macao wa Jamhuri ya Watu wa China, ni jiji la pwani na Mkoa Maalum wa Utawala (SAR) lilio kusini mwa Uchina, likiingilia kati ya Delta ya Mto Pearl kutoka Hong Kong. Kwa eneo la kilomita za mraba 32.9 (maili 12.7), ni mojawapo ya maeneo yenye idadi kubwa ya watu kwa kilomita za mraba duniani, na idadi ya watu inakadiriwa kuwa karibu 700,000. Ikiwa imeorodheshwa kuwa ya 184 kwa ukubwa wa eneo, Macau ina msongamano mkubwa wa watu wa takriban 21,000 kwa kila kilomita ya mraba.
Mkoa wenye utawala wa pekee wa Jamhuri ya Watu wa China 澳門特別行政區 (Kichina) Região Administrativa Especial de Macau da República Popular da China(Kireno) |
|
![]() |
![]() |
Eneo la Macau |
|
Lugha Rasmi | · Kichina · Kireno |
---|---|
Mtendaji mkuu | Ho Iat Seng |
Historia | |
Kuanzishwa kwa mji | Karne ya 5 BK |
Iliundwa na wenyeji Wachina kutwaliwa na Ureno | 1557 |
koloni ya Ureno | 31 Agosti 1862 |
Mkoa mwenye utawala wa pekee wa Jamhuri ya Watu wa China | 20 Desemba 1999 |
Ukubwa wa eneo | |
Jumla | 30.3 km² |
Idadi ya watu | |
Kadirio (2015) | 642,900 |
Sensa (2011) | 552,503 |
Msongamano | 18,568 /km² |
Pato la taifa PPP (2025) | |
Jumla | $98.64 billioni (ya 139) |
Capita | $140,250 |
Pato la taifa (2025) | |
Jumla | $59.27 bilioni (ya ) |
Capita | $84,280 |
Kiashiria cha maendeleo ya watu (2022) | 0.925 (24) Maendeleo ya Juu Sana |
Sarafu | Pataca ya Macau |
Eneo la saa | UTC +8 (MST) |
Nambari ya mwito | +853 |
Jina la kikoa | .mo |
1 Mji mkuu ulikuwa "Cidade do Nome de Deus de Macau" au rasi ya Macau yenyewe; makao makuu ya serikali ya koloni yalikaa kwenye tarafa ya Sao Lorenco. 2 Habari kutoka Direcção dos Serviços de Estatística e Censos (ofisi ya takwimu ya Macau ) |
Tarehe 23 Oktoba 2018 rais wa China Xi Jinping alizindua rasmi daraja la baharini refu kuliko yote duniani (kilometa 55) linalounganisha Hong Kong, Macau na China bara (mji wa Zhuhai).
Koloni la Ureno
Macau ilikuwa kituo cha Ureno tangu karne ya 16 na Wareno wakaikodi tangu mwaka 1670.
Macau kama koloni ilithibitishwa katika Mkataba wa Beijing wa mwaka 1887 kati ya China na Ureno.
Macau kama eneo la pekee la China
Mwaka 1999 ilirudishwa mikononi mwa serikali ya China lakini kwa hali ya pekee inayofanana na ile ya eneo la jirani la Hong Kong.
Hivyo Macau inaendendelea kuratibu yenyewe mambo yake kwa ndani, lakini madaraka kuhusu usalama, jeshi na siasa ya nje yako Beijing.
Watu
Wakazi wengi (88.4%) ni Wachina asilia, 1.8% ni Wareno. Kwa kuwa uzazi ni mdogo sana, kuna wahamiaji wengi, hasa Wafilipino (4.6%) na Wavietnam (2.4%).
Lugha rasmi ni Kichina na Kireno. Katika matumizi ya kawaida, Kichina cha Canton kinaongoza (87.5%), na Kiingereza kina waongeaji wengi (2.8%) kuliko Kireno (0.7%).
Upande wa dini, 58.9% wanafuata dini za jadi za Kichina (mchanganyiko wa Ukonfusio na Utao), 17.3% ni Wabuddha au Watao, 7.2% ni Wakristo. 15.4% hawana dini yoyote.
Uchumi
Uchumi wa Macau hutegemea utalii na hasa michezo ya kamari. Kuna pia viwanda vya nguo.
Tazama pia
Viungo vya nje
- Serikali
- Portal of the government of Macau
- Government Information Bureau
- Macau Yearbook Ilihifadhiwa 14 Septemba 2008 kwenye Wayback Machine.
- Cultural Affairs Bureau
- Gaming Inspection and Coordination Bureau
- Taarifa za jumla
- Macau entry at The World Factbook
- Macau Ilihifadhiwa 7 Juni 2008 kwenye Wayback Machine. from UCB Libraries GovPubs
- Macau katika Open Directory Project
- Macau profile from the BBC News
- Wikimedia Atlas of Macau
- Country Study: Macau from the United States Library of Congress (August, 2000)
- Dr Howard M Scott "Macau"
- Utalii
- Macau Government Tourist Office
- Macau City Guide Ilihifadhiwa 26 Aprili 2009 kwenye Wayback Machine.
- Malezi
- Michezo
Nchi na maeneo ya Asia |
Afghanistan | Armenia2 | Azerbaijan | Bahrain | Bangladesh | Bhutan | Brunei | China | Falme za Kiarabu | Georgia2 | Hong Kong3 | Indonesia | Iraq | Israel | Jamhuri ya China (Taiwan) | Japani | Kamboja | Kazakhstan | Kirgizia | Korea Kaskazini | Korea Kusini | Kupro2 | Kuwait | Laos | Lebanoni | Macau3 | Malaysia | Maldivi | Mongolia | Myanmar | Nepal | Omani | Pakistan | Palestina | Qatar | Saudia | Singapuri | Sri Lanka | Syria | Tajikistan | Timor ya Mashariki | Turkmenistan | Uajemi | Ufilipino | Uhindi | Urusi1 | Uthai | Uturuki1 | Uzbekistan | Vietnam | Yemen | Yordani |
1. Nchi ina maeneo katika Asia na Ulaya. 2. Nchi iko Asia lakini inahesabiwa pia kati ya nchi za Ulaya kwa sababu za historia au utamaduni. 3. Eneo la pekee la China. |
![]() |
Makala hii kuhusu maeneo ya China bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Macau kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.