jimbo la Marekani From Wikipedia, the free encyclopedia
California (/ˌkælɪˈfɔːrnjə/) ni jimbo katika Mkoa wa Magharibi wa Marekani linalopatikana kwenye Pwani ya Pasifiki. Linapakana na Oregon upande wa kaskazini, Nevada na Arizona upande wa mashariki, na linashiriki mpaka wa kimataifa na imbo la Mexico la Baja California upande wa kusini. Pamoja na zaidi ya watu milioni 39 wanaoishi kwenye eneo la maili za mraba 163,696 (km² 423,970), ni jimbo lenye idadi kubwa zaidi ya watu Marekani, la tatu kwa ukubwa kwa eneo, na kitengo cha idadi ya watu kikubwa zaidi kisichokuwa cha taifa barani Amerika Kaskazini.
Jimbo | ||||
---|---|---|---|---|
Kauli Mbiu "Eureka" |
||||
Eneo la California katika Marekani | ||||
Nchi | Marekani | |||
Mwaka wa Kujiunga | Septemba 9, 1850; 174 (31st) (Miaka 175 iliyopita) | |||
Mji/Makao makuu | Sacramento | |||
Jiji kubwa | Los Angeles | |||
Lugha rasmi | Kiingereza | |||
Lugha zinazozungumzwa | 56.8% Kiingereza 28.18% Kihispania |
|||
Utaifa | Mkalifornia Californian (en) | |||
Serikali | ||||
Gavana | Gavin Newsom | |||
Naibu gavana | Eleni Kounalakis (D) | |||
Ukubwa wa eneo | ||||
Jumla | 423970 km² | |||
Ardhi | 403466 km² | |||
Maji | 20504 (4.84%) | |||
Msongamano | auto /km² | |||
Idadi ya Watu | ||||
Mwaka wa Makisio | ||||
Idadi ya watu (makisio) | 39,512,223 | |||
Pato la Taifa | ||||
Mwaka wa Makisio | 2024 | |||
Jumla | $4.08 trilioni (ya 1) | |||
Capita | $93,460 | |||
Kiashiria cha Maendeleo ya Watu (2018) | 0.935 (ya 15) Maendeleo ya Juu Sana |
|||
Mapato ya Kati ya Kaya (2023) | $95,500 () | |||
Eneo la saa | UTC-8 (PST), UTC-7 (PDT) | |||
Tovuti | 🔗www.ca.gov |
Wakazi wamekadiriwa kuwa 39,512,223 mwaka 2019.
California ni kati ya majimbo ya Marekani yenye uwezo mkubwa wa kiuchumi. Kama California ingekuwa nchi huru ya kujitegemea uchumi wake ungekuwa na nafasi ya 8 duniani. Utalii, kilimo na viwanda vya ndege huajiri watu wengi. Kampuni za kompyuta zimestawi vizuri sana California, kwa mfano Microsoft. Los Angeles, hasa eneo la Hollywood, ni kitovu cha kupiga picha za filamu.
Mji mkuu ni Sacramento. Kuna miji 59 yenye wakazi zaidi ya lakhi moja:
Mji | Wakazi | |
1 | Los Angeles | 3.957.875 |
2 | San Diego | 1.305.736 |
3 | San Jose | 944.857 |
4 | San Francisco | 799.263 |
5 | Fresno | 500,017 |
6 | Long Beach | 491.564 |
7 | Sacramento | 452.959 |
8 | Oakland | 412.318 |
9 | Santa Ana | 351.697 |
10 | Anaheim | 345.317 |
Majimbo ya Marekani |
---|
Alabama • Alaska • Arizona • Arkansas • California • Colorado • Connecticut • Delaware • Florida • Georgia • Hawaii • Idaho • Illinois • Indiana • Iowa • Kansas • Kentucky • Louisiana • Maine • Maryland • Massachusetts • Michigan • Minnesota • Mississippi • Missouri • Montana • Nebraska • Nevada • New Hampshire • New Jersey • New Mexico • New York • North Carolina • North Dakota • Ohio • Oklahoma • Oregon • Pennsylvania • Rhode Island • South Carolina • South Dakota • Tennessee • Texas • Utah • Vermont • Virginia • Washington • West Virginia • Wisconsin • Wyoming |
Makala hii kuhusu maeneo ya Marekani bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu California kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.