Senene
From Wikipedia, the free encyclopedia
Senene (jina la kisayansi: Ruspolia differens[1] [2]; jina la Kiganda: Nsenene; jina lililokosewa: "panzi wenye pembe ndefu") ni mdudu wa familia Tettigoniidae katika oda Orthoptera. Wapo tele magharibi mwa Kenya na Tanzania, kusini mwa Uganda na kaskazini mwa Rwanda lakini anapatikana pia Afrika Kusini, Malawi, Cote d'Ivoire, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Ghana, Burundi, Kamerun, Zimbabwe, Zambia, Madagaska pamoja na Mauritius.[3]
Senene | ||||||||||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
Jika la Ruspolia nitidula anayefanana na senene | ||||||||||||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||||||||||
| ||||||||||||||||||||||||
Baada ya majira ya mvua wapevu hukongomana katika makundi ya maelfu ya wadudu.
Spishi aina hii kwa muda mrefu imekuwa ikijulikana kama moja ya totems nyingi za Ufalme wa Buganda wa Uganda. Zilipatikana na Seruwu Douglass kutoka Visiwa vya Ssese huko Masaka.
Mara nyingi wadudu kama senene huitwa panzi, lakini senene wana vipapasio virefu sana kuliko pronoto na jike ana kiungo kama mfuo kinachofanana na kitara kinachotumika kwa kutaga mayai. Kinyume na hivyo panzi wana vipapasio vifupi na majike hawana kiungo kwa umbo la kitara.
Mara nyingi huchanganyikiwa na Ruspolia nitidula inayohusiana kwa karibu.[4][5]