Mlali ni kata ya Wilaya ya Kongwa katika Mkoa wa Dodoma, Tanzania, yenye postikodi namba 41505[1].

Mlali kijiografia ipo kwenye mlima wa kuvutia ambao upo kwenye safu za milima ya Rubeho.

Kwa sasa Mlali inajumuisha vijiji vitatu, Mlali Iyegu, Mlali Bondeni na Ihanda. Mlali Iyegu ni pazuri kwa kutalii kwenye mlima na kujionea wanyama kama nyani, ngedere, gendaheka, digidigi, nyegere n.k.

Katika sensa ya mwaka 2022 wakazi walihesabiwa 28,218 [2]. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 19,623 [3] waishio humo.

Wakazi wengi wanajishughulisha na kilimo (mahindi, alizeti, mbaazi, karanga, n.k.) na ufugaji (ng'ombe, mbuzi, kondoo, kuku, bata, n.k.).

Mlali ni kijiji kinachotegemewa kwa huduma za afya kwa ukanda mkubwa wa wilaya ya Kongwa na wilaya jirani kupitia kituo Cha afya cha Mlali ,lakini pia Mlali kuna kituo cha watoto walemavu ambacho kinasaidia Tanzania nzima na nchi jirani kunyoosha viungo na matibabu mengi ya viungo vya watoto walemavu. Mlali ni mojawapo ya sehemu chache katika mkoa wa Dodoma zinazopata huduma za maji Kwa asilimia kubwa,maji yanayotegemewa na wakazi yanatoka katika mlima mkubwa uliopo Mlali unaotokana na safu za mlima rubeho.

Marejeo

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.