Kameruni, kirasmi Jamhuri ya Kameruni, ni jamhuri ya muungano katika Afrika ya Magharibi.
Jamhuri ya Kameruni | |
---|---|
République du Cameroun (Kifaransa) Republic of Cameroon (Kiingereza) | |
Kaulimbiu ya taifa: Paix – Travail – Patrie (Kifaransa) Peace – Work – Fatherland (Kiingereza) "Amani – Kazi – Nchi" | |
Wimbo wa taifa: Chant de Ralliement | |
Mahali pa Kamerun | |
Mji mkuu | Yaunde |
Mji mkubwa nchini | Duala |
Lugha rasmi | |
Serikali | Jamhuri yenye mdikteta |
• Rais • Waziri Mkuu | Paul Biya Joseph Dion Ngute |
Eneo | |
• Eneo la jumla | km2 475 440[1] |
• Maji (asilimia) | 0.57[1] |
Idadi ya watu | |
• Kadirio la 2023 | 30 135 732[1] |
Pato la taifa | Kadirio la 2023 |
• Jumla | USD bilioni 49.262[2] |
• Kwa kila mtu | 1 721[2] |
Pato halisi la taifa | Kadirio la 2023 |
• Jumla | USD bilioni 133.335[2] |
• Kwa kila mtu | USD 4 660[2] |
Maendeleo (2021) | 0.576[3] - wastani |
Sarafu | Faranga ya CFA |
Majira ya saa | UTC+1 (Afrika Magharibi) |
Upande wa magari | Kulia |
Msimbo wa simu | +237 |
Msimbo wa ISO 3166 | CM |
Jina la kikoa | .cm |
Imepakana na Nijeria, Chadi, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Jamhuri ya Kongo, Gabon, Gine ya Ikweta na Ghuba ya Gine.
Lugha rasmi na lugha za taifa ni Kifaransa (kinachoongoza kwa zaidi ya asilimia 80) na Kiingereza.
Jiografia
Maeneo kiutawala
Kameruni imegawiwa katika mikoa (regions) 10 na wilaya (départements) 58.
Mikoa ni:
- Mkoa wa Adamawa,
- Mkoa wa Kati,
- Mkoa wa Mashariki,
- Mkoa wa Kaskazini ya Mbali,
- Mkoa wa Pwani,
- Mkoa wa Kaskazini,
- Mkoa wa Kaskazini-Magharibi,
- Mkoa wa Magharibi,
- Mkoa wa Kusini, na
- Mkoa wa Kusini-Magharibi
Ona pia: Orodha ya miji ya Kameruni
Historia
Historia ya awali
Katika karne za BK Wabantu wenye ujuzi wa kilimo na uhunzi walianza uenezi wao kutoka huko kwenda kutawala maeneo mengi ya Afrika ya Kati, Kusini mwa Afrika na Afrika Mashariki.
Wakati wa ukoloni
Kameruni ilikuwa koloni la Ujerumani hadi Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia. Baada ya Ujerumani kushindwa vita, nchi ikagawiwa kati ya Uingereza na Ufaransa chini ya mamlaka ya Shirikisho la Mataifa kama eneo la kudhaminiwa.
Tangu uhuru hadi leo
Mwaka wa 1960, Wafaransa waliacha Kameruni ikawa nchi huru. Wananchi wa Kameruni ya Kiingereza walipiga kura kuamua kama walitaka kuwa sehemu ya Nigeria au ya Kameruni. Kaskazini wengi walipendelea kukaa Nigeria, hivyo maeneo hayo sasa ni sehemu ya Nigeria. Wananchi wengi wa kusini waliamua wajiunge na Kameruni[4]. Kwa kusudi la kuheshimu tofauti za kiutamaduni kulikuwa na katiba mpya kwenye mwaka 1961 Shirikisho la Jamhuri ya Kameruni.
Tangu 1972 muundo wa nchi ulibadilishwa kuacha mfumo wa shirikisho na kuwa jamhuri ya muungano inayokazia zaidi matumizi ya lugha ya Kifaransa ingawa Kiingereza bado ni moja ya lugha rasmi. Jina la nchi pia likabadilishwa kuwa Jamhuri ya Muungano ya Kameruni mwaka wa 1972. Hapo sehemu ya Wakamerun wanaotumia lugha ya Kiingereza walijisikia kuwa wananyimwa haki zao.[5] Baadaye, mwaka wa 1984 jina likabadilishwa tena kuwa Jamhuri ya Kameruni (kwa Kifaransa République du Cameroun).
Tangu mwaka 2016 upinzani uliongezeka kati ya watu wa magharibi wanaotumia Kiingereza. Harakati hiyo ilijibiwa na serikali na polisi kwa ukali na hii umeleta kuanzishwa kwa wanamgambo wenye silaha wanaoshambulia polisi na jeshi la serikali kuu. Tangu mwaka 2017 wapinzani wamedai uhuru wa sehemu yenye lugha ya Kiingereza wakitangaza wameunda nchi mpya ya "Ambazonia". Serikali iliundwa inayokaa Nigeria; lakini kuna vikundi tofauti ambavyo wanapigana kati yao[6]. Nchi hii haitambuliwi kimataifa. Mwaka 2021 kulikuwa na majadiliano kuhusu amani kati kundi linalojiita serikali ya Ambazonia na serikali ya Kameruni[7], lakini makundi mengine yaliendelea na mapigano ya silaha[8].
Siasa
Uchumi
Watu
Wakazi walikuwa 22,534,532 mwaka 2013, ambao wamegawanyika sawasawa kati ya wanaoishi mijini na wale wa vijijini.
Lugha rasmi ni Kifaransa pamoja na Kiingereza. Hata hivyo wakazi wanaongea pia lugha za makabila yao mengi.
Upande wa dini, 70% ni Wakristo (40% Wakatoliki na 30% Waprotestanti), 18% ni Waislamu, 3% ni wafuasi wa dini asilia za Kiafrika. 6% hawana dini yoyote.
Utamaduni
Elimu
Tazama pia
- Ukristo nchini Kameruni
- Kanisa Katoliki nchini Kameruni
- Uislamu nchini Kameruni
- Mawasiliano nchini Kameruni
- Mambo ya kigeni ya Kameruni
- Orodha ya miji ya Kameruni
- Jeshi la Kameruni
- Usafirishaji nchini Kameruni
- Chama cha Wanaskauti Kameruni
- Orodha ya nchi kufuatana na wakazi
- Orodha ya nchi za Afrika kulingana na idadi ya watu
- Orodha ya nchi za Afrika kulingana na msongamano wa watu
- Orodha ya nchi za Afrika kulingana na pato la taifa
- Demografia ya Afrika
Marejeo
Viungo vya nje
Wikiwand in your browser!
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.