Cabo Verde
From Wikipedia, the free encyclopedia
Cabo Verde (Kiingereza: Cape Verde) ni nchi ya visiwa katika bahari ya Atlantiki mbele ya pwani ya Afrika ya Magharibi.
Jamhuri ya Cabo Verde República de Cabo Verde (Kireno) | |
---|---|
Kaulimbiu: Unidade, Trabalho, Progresso (Kireno) "Umoja, Kazi, Maendeleo" | |
Wimbo wa taifa: Cântico da Liberdade (Kireno) "Mkarara wa Uhuru" | |
Mji mkuu na mkubwa | Praia |
Lugha rasmi | Kireno Kikaboverde |
Serikali | Jamhuri |
• Rais • Waziri Mkuu | José Maria Neves Ulisses Correia e Silva |
Eneo | |
• Jumla | km2 4 033[1] |
Idadi ya watu | |
• Kadirio la 2023 | 603 901[1] |
PLT (PPP) | Kadirio la 2023 |
• Jumla | USD bilioni 5.717[2] |
• Kwa kila mtu | USD 9 909[2] |
PLT (kawaida) | Kadirio la 2023 |
• Jumla | USD bilioni 2.598[2] |
• Kwa kila mtu | USD 4 503[2] |
HDI (2021) | 0.662[3] - kati |
Sarafu | Escudo ya Cabo Verde |
Jiografia
Eneo la visiwa vyake kwa jumla ni km² 4,033.
Funguvisiwa lake lina visiwa 15 katika vikundi viwili:
- Visiwa "juu ya upepo" (Barlavento): Santo Antão, São Vicente, São Nicolau, Sal, Boa Vista na visiwa bila watu vya Santa Luzia, Branco na Razo.
- Visiwa "chini ya upepo" (Sotavento): Maio, Santiago, Fogo, Brava na visiwa bila watu vya Ilheus Secos ou do Rombo.
Miji
Mji mkuu ni Praia katika kisiwa cha Santiago.
Miji mikubwa zaidi ni (takwimu za mwaka 2010): Praia (wakazi 127,832), Mindelo (wakazi 70,468), Santa Maria (wakazi 23,839), Assomada (wakazi 12,026), Pedra Badejo (wakazi 9,345) na São Filipe (wakazi 8,125).
Historia
Hadi kufika kwa Wareno katika karne ya 15 visiwa vya Cabo Verde havikuwa na watu.
Wareno walianzisha mashamba ya miwa na kuleta watumwa kutoka bara la Afrika.
Cabo Verde ilikuwa pia kituo muhimu cha biashara ya watumwa kati ya Afrika na Amerika.
Wahamiaji kutoka Ulaya walikuwa pia Wahispania, Waitalia pamoja na Wayahudi na Waislamu waliokataliwa kukaa kwao Ureno.
Watu
Kutokana na historia hiyo, leo idadi kubwa ya wakazi ni machotara waliozaliwa na Waafrika (waliochangia 56% ya DNA) na Wazungu (waliochangia 44%).
Lugha rasmi ni Kireno, lakini wakazi wanazungumza zaidi aina mbalimbali za Krioli iliyotokana na lugha hiyo.
Upande wa dini, walau 89.1% ya wakazi ni Wakristo, hasa wa Kanisa Katoliki (78.7%), lakini pia wa madhehebu mbalimbali ya Uprotestanti (10.4%).
Kutokana na hali ngumu ya uchumi, wananchi wanaoishi nje ya Cabo Verde ni mara mbili kuliko wale wanaoishi nchini. Kati ya waliohama baada ya uhuru (1975), 500,000 wanaishi Marekani na 150,000 Ureno. Hata hivyo kuna wahamiaji vilevile, hasa kutoka nchi za Afrika bara.
Tazama pia
Marejeo
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.