kilabu ya mpira huko London, Uingereza From Wikipedia, the free encyclopedia
Chelsea Football Club[5][6] [7][8]ni klabu ya mpira wa miguu ya nchini Uingereza iliyo na maskani yake Fulham, London. Klabu hii ilianzishwa mwaka 1905, na kwa miaka mingi sana imekuwa ikishiriki ligi kuu ya Uingereza. Uwanja wao wa nyumbani ni Stamford Bridge ambao una uwezo wa kuingiza watazamaji 41,837, wameutumia uwanja huu tangu klabu ilivyoanzishwa.
Jina kamili | Chelsea Football Club | |||
---|---|---|---|---|
Jina la utani | The Blues The Pensioners (zamani)[1] | |||
Imeanzishwa | 10 Machi 1905[2] | |||
Uwanja | Stamford Bridge (Uwezo: 40,341[3][4]) | |||
Mmiliki | Todd Boehly Clearlake Capital Hansjörg Wyss Mark Walter | |||
Mwenyekiti | Todd Boehly | |||
Kocha | Enzo Maresca | |||
Ligi | Ligi Kuu Uingereza (EPL) | |||
Tovuti | tovuti ya klabu | |||
Mfungaji bora wa muda wote | Frank Lampard | |||
|
Chelsea, kwa mara ya kwanza ilipata mafanikio makubwa mwaka 1955, ambapo walipata ubingwa wa ligi, na walishinda mataji kadhaa katika miaka ya 1960, 1970, 1990 na 2000. Klabu hii imefurahia zaidi mafanikio katika miongo miwili ilopita, kwa kushinda mataji makubwa 15 tangu mwaka 1997.
Nyumbani, Chelsea imeshinda ubingwa wa ligi mara nne, kombe la FA mara saba, kombe la ligi mara nne, pamoja na ngao za jamii mara nne. Na kimataifa Chelsea imeshashinda UEFA Cup Winners' Cups mara mbili, UEFA Super Cup moja, UEFA Europa League mara mbili na UEFA Champions League mara mbili. Chelsea ndio klabu pekee kutoka London kushinda UEFA Champions League, na ni moja kati ya klabu nne kutoka Uingereza, kuchukua makombe yote makubwa matatu ya Ulaya.
Kwa kawaida Chelsea huvaa jezi ya bluu, kaptula ya bluu na soksi nyeupe. Nembo ya klabu imebadilishwa mara nyingi kulingana na wakati na kuboresha muonekano wa klabu. Nembo ya sasa inaonesha picha ya simba akiwa amebeba mkuki. Tangu Julai 2003, Chelsea imekuwa ikimilikiwa na bilionea wa Kirusi, Roman Abramovich. Tarehe 7 Mei 2022, Chelsea ilithibitisha kwamba masharti yametimiza na kikundi kipya cha umiliki, kinachoongozwa na Todd Boehly, Clearlake Capital, Mark Walter na Hansjörg Wyss, kununua klabu hiyo.[9] Mnamo tarehe 25 Mei 2022, serikali ya uingereza iliidhinisha kuuzwa kwa Chelsea kwa £4.25bn. Mnamo tarehe 30 Mei 2022, mauzo yalikamilika, na hivyo kumaliza umiliki wa miaka 19 wa Abramovich.[10]
Kama ilivyokuwa tarehe 10 Agosti 2022, kulingana na vyanzo mseto katika tovuti rasmi.[11]
Note: Flags indicate national team as has been defined under FIFA eligibility rules. Players may hold more than one non-FIFA nationality.
|
|
Note: Flags indicate national team as has been defined under FIFA eligibility rules. Players may hold more than one non-FIFA nationality.
|
|
|
|
Chanzo: Chelsea F.C.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.