Romania (kwa Kiromania: România) ni nchi ya Ulaya ya kusini-mashariki.
| |||||
Kaulimbiu ya taifa: -- | |||||
Wimbo wa taifa: Deşteaptă-te, române! | |||||
Mji mkuu | Bukarest (Bucureşti) | ||||
Mji mkubwa nchini | Bukarest | ||||
Lugha rasmi | Kiromania | ||||
Serikali Rais Waziri Mkuu |
Jamhuri Klaus Iohannis Marcel Ciolacu | ||||
Uhuru Ilitangazwa ilitambiluwa |
9 Mei 1877 (Kalenda ya Juliasi)2 13 Julai 18783 | ||||
Eneo - Jumla - Maji (%) |
238,391 km² (ya 82) 3 | ||||
Idadi ya watu - 2021 kadirio - 2011 sensa - Msongamano wa watu |
19,186,201[1][2] (ya 61) 19,599,506[3][4] 80.4/km² (ya 118) | ||||
Fedha | Leu (RON ) | ||||
Saa za eneo - Kiangazi (DST) |
EET (UTC+2) EEST (UTC+3) | ||||
Intaneti TLD | .ro | ||||
Kodi ya simu | +40
- | ||||
1Lugha kama Kihungaria, Kijerumani, Kiromani, Kiukraine na Kiserbia hutumiwa kieneo kwenye ngazi kadhaa 2 Vita ya uhuru wa Romania. |
Imepakana na Hungaria, Serbia, Ukraine, Moldova na Bulgaria.
Ina pwani kwenye Bahari Nyeusi ambako unaishia mto Danube.
Historia
Homo sapiens aliishi katika eneo hilo walau kuanzia miaka 40,000 iliyopita.
Kabla ya kutekwa na Warumi mwanzoni mwa karne ya 2, walikuwepo makabila ya Wathraki, hasa Wadacha na Wagete.
Chini ya Dola la Roma kwa miaka 165 kulikuwa na wahamiaji wengi walioingiza lugha ya Kilatini.
Baadaye nchi ilitekwa na makabila mengine mbalimbali.
Katika karne za kati kulikuwa na falme ndogo tatu: Wallachia, Moldavia na Transilvania, nazo ziliendelea kuwa na madaraka fulani hata chini ya Dola la Osmani hadi karne ya 18 au 19.
Romania ilianzishwa mwaka 1859 kwa kuunganisha Moldavia na Wallachia ikapewa jina hilo mwaka 1866, ikajikomboa kutoka dola la Osmani mwaka 1877.
Kutokana na vita vikuu vya kwanza, Transilvania, Bukovina na Besarabia viliungana na Ufalme wa Romania.
Katika vita vikuu vya pili, Romania iliunga mkono Ujerumani dhidi ya Muungano wa Kisovieti hadi mwaka 1944.
Wakomunisti waliteka nchi na baada ya vita kwisha, Romania ilipoteza maeneo mbalimbali na kulazimishwa kujiunga na Mapatano ya Warshawa kama jamhuri ya kisoshalisti.
Baada ya mapinduzi ya mwaka 1989, Romania ilielekea demokrasia na uchumi wa soko huria.
Baada ya kujiunga na Umoja wa Ulaya mwaka 2007, Romania imeanza kustawi na kwa sasa inaongoza pamoja na Malta zikiwa na ongezeko la 5% kwa mwaka.
Watu
Romania ina wakazi 19,679,306 katika eneo la km² 238.391. Idadi yao inazidi kupungua.
Lugha rasmi ya nchi nzima ni Kiromania ambayo ni lugha ya Kirumi kama Kiitalia, Kifaransa na Kihispania, lakini lugha nyingine kadhaa zinatambuliwa na sheria, kuanzia Kihungaria.
Wakazi wengi ni Wakristo, hasa Waorthodoksi (81%), wakifuatwa na Waprotestanti (6.2%) na Wakatoliki (5.1%).
Tazama pia
Tanbihi
Wikiwand in your browser!
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.