Zohali
From Wikipedia, the free encyclopedia
Zohali ni sayari ya sita kutoka Jua katika Mfumo wa Jua. Ni sayari kubwa ya pili baada ya Mshtarii.
Ukweli wa haraka Jina, Asili ya jina ...
Zohali | |
---|---|
Picha ya Zohali na bangili zake kutoka Cassini. | |
Jina | |
Asili ya jina | Kar. زحل (zuḥal) |
Majina mengine | Zuhali, Zohari Saturn (Kng.) |
Alama | |
Tabia za njiamzingo | |
Umbali mfupi | km 1,352,550,000 au 9.0412 |
Umbali mrefu | km 1,514,500,000 au 10.1238 |
km 1,433,530,000 au 9.5826 | |
Uduaradufu | 0.0565 |
siku 10,755.70 miaka 29.4475 | |
Mwinamo | 2.485° toka njia ya Jua |
Miezi | 146 |
Tabia za kimaumbile | |
km 58,232 mara 9.123 ya Dunia | |
Tungamo | kg 5.6834×1026 mara 95.159 ya Dunia |
g/cm3 0.687 | |
Uvutano wa usoni | m/s2 10.44 |
Kasi ya kuponyokea | km/s 35.5 |
saa 10.5433 | |
saa 10.5606 | |
Weupe | 0.342 (Bond) 0.499 (jiometri) |
Halijoto | K 134 (−139.15°C) |
Funga
Inaonekana kwa macho matupu si lazima kutumia darubini. Kwa hiyo imeshajulikana tangu zamani ilitambuliwa na wataalamu wa nyakati za kale.
Uso wa Zohali hauonekani kwa sababu angahewa nzito inafunika kila sehemu. Mada ya angahewa ni hasa hidrojeni. Kutokana na uzito wa angahewa shinikizo ndani yake inaongezeka sana katika vilindi vyake na kusababisha gesi za angahewa kuingia katika hali ya giligili inayobadilika kuwa mango hadi metali ndani zaidi.