![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/0/0b/Positive_angle.svg/langsw-640px-Positive_angle.svg.png&w=640&q=50)
Nyuzi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Nyuzi (pia: digrii kutoka neno la Kiingereza) ni kizio cha kupimia pembe . Msingi wake ni mzunguko kamili wa duara unaogawiwa kwa sehemu 360. Kwa kawaida nyuzi moja huandikwa kama 1°.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/0/0b/Positive_angle.svg/640px-Positive_angle.svg.png)
Nusuduara ina 180°. Pembemraba ina 90°. Jumla ya pembe ndani ya pembetatu ni 180°, ndani ya mstatili ni 360°.
Nyuzi inaweza kugawiwa tena kwa dakika na sekunde ya tao. Dakika ya tao ni sehemu ya 60 na sekunde ya tao ni sehemu ya 3600 ya nyuzi moja.