Wernher von Braun
From Wikipedia, the free encyclopedia
Wernher Magnus Maximilian von Braun (23 Machi 1912 - 16 Juni 1977) [1] alikuwa mhandisi na mwanasayansi kutoka nchini Ujerumani . Alikuwa mbuni wa roketi kuanzia miaka ya 1930 hadi 1972. [2] Ametajwa kama mhandisi muhimu zaidi wa roketi katika karne ya 20. [3] Alifanya kazi kwa serikali na jeshi la Ujerumani wakati wa Vita vya Kidunia vya pili akajiunga pia na shirika la SS. Baada ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia alipelekwa Marekani kama mfungwa wa vita akaendelea kufanya kazi kwa jeshi la Marekani na NASA. Mnamo 1955 von Braun alipata kuwa raia wa Marekani.
Alikuwa mbuni mkuu wa roketi ya V-2, iliyokuwa roketi ya kwanza kuruka hadi anga-nje. [4] Baadaye alibuni roketi ya Saturn V iliyowapeleka wanaanga wa Apollo 11 hadi mwezini mnamo 1969. [1]