Schutzstaffel - SS
From Wikipedia, the free encyclopedia
Schutzstaffel (Kikosi cha ulinzi) -kwa kifupi SS- ilikuwa jina la kitengo cha Chama cha Nazi au NSDAP nchini Ujerumani kilichoanzishwa mwaka 1925kama kundi la walinzi wa kiongozi wa chama Adolf Hitler. SS ilishiriki katika maangamizi makuu dhidi ya Wayahudi wa Ulaya na kutawala makambi ya mauti. Kutoka kundi dogo la walinzi wa binafsi iliendelea kuwa tawi la kijeshi la Chama cha Nazi lililoshiriki pia kwenye mapigano ya Vita Kuu ya Pili ya Dunia. Ikapigwa marufuku kama chama cha kihaini mwaka 1945.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/5/5c/Schutzstaffel_SS.png/320px-Schutzstaffel_SS.png)