![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/d/dc/20_Schistosoma_mansoni.tif/lossy-page1-640px-20_Schistosoma_mansoni.tif.jpg&w=640&q=50)
Mnyoo-kichocho
From Wikipedia, the free encyclopedia
Minyoo-kichocho ni spishi za minyoo vidusia za jenasi Schistosoma zinazosababisha ugonjwa wa kichocho kwa watu. Spishi zinaweza kugawanywa katika vikundi viwili kwa njia mbili tofauti. Njia ya kwanza ni mgawanyiko kulingana na ogani ambamo wapevu wanaishi, matumbo au kibofu. Njia ya pili ni kulingana na mahali pa mwiba kwenye mayai, kwa upande au kwenye ncha.
Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Mnyoo-kichocho | ||||||||||||||||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
![]() | ||||||||||||||||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||||||||||||||||
| ||||||||||||||||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||||||||||||||||
Spishi 6 za minyoo-kichocho:
| ||||||||||||||||||||||||||||
Funga
Spishi nyingine za Schistosoma huambukiza vertebrata wengine.
Minyoo wa familia Schistosomatidae hutofautiana na minyoo-bapa wengine kwa kuwa wana jinsia mbili tofauti ambazo zina ukubwa tofauti. Wana vidusiwa wawili, kidusiwa cha kati (konokono) na kidusiwa cha mwisho (vertebrata). Wanafika hatua ya upevu katika damu ya kidusiwa cha mwisho.