From Wikipedia, the free encyclopedia
Vertebrata ni jina la kitaalamu la kutaja wanyama wote wenye uti wa mgongo. Mifano ni mamalia, ndege (Aves), reptilia (wanyama watambaaji kama nyoka au mamba) na samaki. Mwanadamu pia huhesabiwa humo kibiolojia.
Vertebrata | ||||||
---|---|---|---|---|---|---|
Mjusi ni mfano wa vertebrata | ||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||
| ||||||
Ngazi za chini | ||||||
Ngeli 9 (uainisho wa kimila):
| ||||||
Vertebrata wana kiunzi cha ndani, neva kuu zinapitishwa ndani ya uti wa mgongo zinapohifadhiwa ndani ya ganda la mfupa. Kuna kitovu cha neva upande wa juu ya uti wa mgongo na kwa wanyama walioendelea zaidi kitovu hiki kimeendelea kuwa ubongo unahifadhiwa ndani ya fuvu.
Vertebrata wako kote duniani kwenye mabara yote na aina mbalimbali za mazingira kuanzia nchi kavu, baharini hadi tako la bahari na hewani (ndege). Takriban spishi 58.000 zinajulikana. Ni wanyama wakubwa maana wanyama wasio na uti wa mgongo kwa jumla ni wadogo zaidi hadi wadogo sana.
Wikispecies has information related to: Vertebrata |
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.