Kichocho
From Wikipedia, the free encyclopedia
Kichocho, kisalisali au kisonono cha damu (pia schistosomiasis au bilharzia) ni ugonjwa ambao minyoo midogo ya aina ya Schistosoma (minyoo-kichocho) inaingia mwilini na kusababisha mwasho wa ngozi katika viungo mbalimbali, homa, udhaifu na baada ya muda damu katika kinyesi au mkojo na maumivu tumboni. [1]