![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/6/61/Orion_Service_Module.jpg/640px-Orion_Service_Module.jpg&w=640&q=50)
Orion (chombo cha angani)
From Wikipedia, the free encyclopedia
Orion ni chombo cha angani kinachotengenezwa na kampuni ya Lockheed Martin kwa ajili na NASA na ESA. Inakusudiwa kubeba hadi wanaanga sita mpaka Mwezi na hata sayari ya Mirihi. Kazi ya kuipanga ilianza mwaka 2005. Chombo cha Orion kitazinduliwa kwa roketi ya Space Launch System inayotarajiwa kupatikana mnamo mwaka 2021 [1].
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/6/61/Orion_Service_Module.jpg/640px-Orion_Service_Module.jpg)
Orion ambayo ni sehemu ya kubeba wanaanga inaunganishwa na kitengo cha huduma penye injini, tangi, betri na teknolojia ya kusafisha hewa (European Service Module) iliyopangwa na ESA na kutengenezwa na Airbus huko Ujerumani[2].
Safari zake zimepangwa kutoka kwenye kituo cha Kennedy Space Center huko Cape Canaveral, Florida, Marekani.
Kwa asili Orion ilipangwwa kwa mradi wa "Constellation" ya NASA iliyofutwa mnamo 2011. Katika mradi mpya Orion ilibaki lakini sasa inatarajiwa kurushwa kwa roketi mpya ya Space Launch System inayolenga kupeleka wanaanga hadi Mwezi na Mirihi hadi mwaka 2033. [3]