From Wikipedia, the free encyclopedia
Mtakatifu Kizito (1872 - Namugongo, Uganda, 3 Juni 1886) ni mmojawapo wa Wafiadini wa Uganda, mdogo kuliko wote.
Alichomwa moto kwa ajili ya imani yake kwa Yesu Kristo akiwa na umri wa miaka 14 tu. Kidogo tu kabla hajauawa alibatizwa na katekista Karolo Lwanga.
Pamoja na wenzake alitangazwa na Papa Benedikto XV kuwa wenye heri tarehe 6 Juni 1920, halafu na Papa Paulo VI kuwa mtakatifu tarehe 18 Oktoba 1964 huko Roma.
Sikukuu yake ni tarehe 3 Juni kila mwaka[1].
Ni msimamizi wa watoto na wa shule za msingi.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.