Tambarare kuu za Marekani
From Wikipedia, the free encyclopedia
From Wikipedia, the free encyclopedia
Tambarare kuu za Marekani (kwa Kiingereza: Great Plains) ni eneo kubwa la nchi hiyo lisilo na milima katika sehemu za kati na za magharibi za Marekani. Sehemu ya kaskazini inaingia ndani ya Kanada.
Upande wa magharibi zinaishia kwenye milima ya Rocky Mountains. Upande wa mashariki tambarare hizi zinapakana na maeneo ambako usimbishaji unaruhusu kustawi kwa misitu.
Majimbo yafuatayo ni sehemu za tambarare kuu:
Tabianchi huwa na miezi ya joto kali pamoja na miezi ya baridi sana. Uoto asilia wa nchi ulikuwa manyasi tu, maana mvua haitoshi kwa miti mingi.
Kabla ya kuja kwa Wazungu huko Marekani, tambarare kuu zilikuwa na ng'ombe mwitu aina ya baisoni kwa mamilioni waliowindwa na Maindio wahamaji na kuwa chakula chao kikuu.
Baisoni waliuawa kwa makusudi na Wamarekani weupe waliotaka kuondoa msingi wa kiuchumi wa Maindio na kutumia maeneo yao kwa kilimo. Sasa ni kitovu cha mazao ya nafaka kama mahindi na ngano ambazo hulisha mifugo na watu.
Makala hii kuhusu eneo fulani bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu eneo hilo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Je, unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.
|
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.