From Wikipedia, the free encyclopedia
Uoto asilia (au Uoto wa asili) ni mimea yote inayoota kiasili, tofauti na ile inayooteshwa na binadamu. Kwa hali hiyo uoto wa asili huhusiana moja kwa moja na tabia ya nchi, kwa mfano nyasi, msitu, vichaka na mbuga.
Msitu ni mkusanyiko wa miti mirefu na mikubwa ambayo huota sehemu kubwa kwa kukaribiana na vichaka ambavyo ni miti midogomidogo na mifupi iliyokusanyika kwa pamoja sana na mbuga ni uoto wa kisavana ambao ni kama nyasi.
Uoto wa asili ni matokeo ya athari za hali ya hewa, ambayo nayo huhusiana na kuathiriwa na sura ya nchi. Kwa mfano misitu minene hustawi katika sehemu za milima zenye mvua nyingi.
Aina na kiasi cha uoto wa asili hubadilika kadiri mvua inavyobadilika. WUtunzaji wa uoto wa asilia ni njia bora ya kuwezesha maisha ya afya katika jamii kwa maana kupitia njia mbalimbali za uoto wa asili kuna mvua, hewa nzuri, makazi ya wanyama. na kama utunzaji wetu wa uoto wa asilia utakuwa bora, basi utatusaidia sisi pamoja na vizazi vijavyo mbeleni.
Makala hii kuhusu mambo ya biolojia bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Uoto asilia kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.