Dar es Salaam
From Wikipedia, the free encyclopedia
Dar es Salaam ni jiji kubwa kuliko yote nchini Tanzania. Pia ni jina la mkoa wake. Dar es Salaam ni mji mkongwe na wenye watu wengi zaidi katika Jumuia ya Afrika Mashariki. Katika Tanzania ndio mji wenye vitega uchumi vingi na ndio mji unaoangaliwa na watu wengi.Dar es Salaam pia ni bandari ya pili kwa ukubwa katika Afrika Mashariki.
Dar es Salaam | |||
![]() |
|||
| |||
![]() |
|||
Majiranukta: 6°48′0″S 39°17′0″E | |||
Nchi | Tanzania | ||
---|---|---|---|
Mkoa | Dar es Salaam | ||
Tarafa | 12 | ||
Kata | 102 | ||
Mitaa | 565 | ||
Serikali[1] | |||
- Aina ya serikali | Jiji | ||
- Mstahiki Meya | Omary S. Kumbilamoto | ||
- Mkurugenzi wa Jiji | Jumanne K. Shauri | ||
Idadi ya wakazi (2022)[2]: 74 | |||
- Wakazi kwa ujumla | 5,383,728 | ||
EAT | (UTC+3) | ||
Msimbo wa posta | 11xxx | ||
Kodi ya simu | 022 | ||
ISO namba | TZ-02 | ||
Tovuti: Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam |
Ni mji mkuu wa kibiashara wa Tanzania wakati Dodoma ni mji mkuu wa Tanzania (kinadharia tangu mwaka 1973). Mpango wa kuhamishia serikali mjini Dodoma unaendelea kwa kasi chini ya rais John Magufuli, japokuwa bado ofisi kadhaa za serikali, ikiwa ni pamoja na Ikulu, zipo Dar es Salaam.
Mji una wakazi wapatao 5,383,728 kwa hesabu ya sensa iliyofanyika katika mwaka wa 2022[3].
Jina

Jina la Dar es Salaam linatoka katika Kurani ambako linamaanisha mahali patulivu au hata paradiso. Surah Al-Anam (Korani 6:127) ina maneno لَهُمْ دَارُ السَّلَامِ عِندَ رَبِّهِمْ lahum dāru as-salāmi `inda rabbihim[4] yanayomaanisha "Hao watapata nyumba ya salama kwa Mola Mlezi wao."[5] . Jina linafanywa na maneno mawili ya Kiarabu; دار dar inayomaanisha "nyumba, jengo, makazi, eneo", "es" ni silabi ya kuunganisha sehemu za jina linalounganishwa na maneno mawili[6], سلام salaam inamaanisha "amani, raha, usalama".

Mara nyingi jina limetafsiriwa kama "Bandari ya Amani" lakini hii ni kosa kutokana na kuchanganya maneno ya Kiarabu دار "dar" (nyumba) na بندر "bandar" (bandari) maana kwa matamshi ya Kiswahili tofauti ya tahajia katika Kiarabu haitambuliki.
Jina la Daressalaam limetumiwa kwa maumbo tofauti kwa mahali mbalimbali katika mazingira ya Kiislamu, kwa mfano huko Brunei Darussalaam, Dar El Salam (Misri), Dar os Salam (Iran), pia kama majina ya taasisi mbalimbali.
Historia
Katika eneo la jiji hili zamani kulikuwa vijiji kadhaa [7]. Sultani Seyyid Majid wa Zanzibar aliamua kujenga ikulu ya pili barani kando ya Mzizima akachagua jina "Dar es Salaam". Hadi leo kuna majengo mawili yaliyobaki ya vyanzo hivi ambayo ni Boma la Kale na Nyumba ya Atiman.
Dar es Salaam ilichaguliwa na wakoloni Wajerumani kuwa mji mkuu wa Afrika ya Mashariki ya Kijerumani kwa sababu ya bandari asilia yenye mdomo mpana wa mto Kurasini. Hivyo kuanzia mwaka 1891 Dar es Salaam ilichukua nafasi ya Bagamoyo kama makao makuu ya utawala.
Bandari pamoja na ujenzi wa reli ya kati kwenda Kigoma tangu mwaka 1904 viliimarisha nafasi ya mji ulioendelea kama mji mkuu baada ya Tanzania bara ya leo kuwa eneo lindwa la Tanganyika chini ya Uingereza.
Utawala
Utawala wa Dar es Salaam uliona mabadiliko kadhaa ambapo mwanzoni mji ulitawaliwa na halmashauri yake na baadaye serikali ya kitaifa ilichukua utawala mikononi mwake au kuukabidhi kwa tume ya serikali[8].
Mwaka 2000 eneo la jiji liligawanywa kwa mamlaka tofauti ambazo mwanzoni zilikuwa nne, ambazo zilikuwa manisipaa za Ilala, Temeke na Kinondoni. Baadaye Ubungo na Kigamboni zilikuwa manisipaa za pekee, kila moja na halmashauri yake. Kwa jiji lote Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam iliundwa. Kwa hiyo hadi 2021 Dar es Salaam ilikuwa na Halmashauri 6.
- Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam
- Halmashauri ya Manispaa ya Ilala
- Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni
- Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni
- Halmashauri ya Manispaa ya Temeke
- Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo
Kwenye Februari 2021 Halmashauri ya Dar es Salaam ilivunjwa na serikali, na Ilala ilibadilishwa jina kuwa Dar es Salaam[9].
Wakazi na uchumi
Dar es Salaam inakadiriwa kuwa na wakazi wapatao milioni tatu. Ingawa Dodoma inafahamika kama ndio mji mkuu wa Tanzania, Dar es Salaam ndiko ziliko ikulu, mabalozi, mashirika ya kimataifa, n.k.
Uwanja wa ndege mkuu wa Tanzania uko pia mjini hii ni Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere.
Bandari ya Dar es Salaam katika bahari ya Hindi, ndio bandari kubwa nchini Tanzania inayojihusisha na usafirishaji na uingizaji wa bidhaa mbalimbali za kilimo, ufugaji, ujenzi, magari, madawa, n.k.
Kiutawala, Dar es Salaam imegawanywa katika manisipaa za Temeke, Ilala, Kinondoni, Kigamboni na Ubungo.
Wakazi na uchumi

Dar es Salaam ni mji unaosemekana kuwa mkubwa kuliko yote kwa sababu ya maendeleo mbalimbali ya viwanda, uwepo wa bahari, uwepo wa sehemu mbalimbali za kihistoria n.k.
Huduma za jiji
Huduma ya maji Dar es Salaam imekuwa na tatizo kubwa katika kudhibiti mfumo wa maji taka katika mkoa wa Dar es Salaam kwa muda mrefu. Tangu shirika la maji DAWASCO (Dar es Salaam Water Supply Company) lilipowekwa rasmi kama shirika husika katika kuratibu utaratibu mzima wa mfumo wa maji safi na maji taka, kumekuwa na nafuu kidogo tu, lakini baada ya muda, liliibuka tatizo la kuibiwa kwa mabomba na uharibifu wa vyanzo mbalimbali vya maji.
Elimu
Kwenye suala hili la elimu vijana wanatakiwa kupewa elimu; hasa vijana wa mitaani wasioingiza kipato inabidi wapewe elimu kwa kazi fulani ili waweze kuajiriwa na kulipa faida taifa kwa kuingizia kipato na kukuza uchumi wa taifa. Mfano wa kazi hizo ni kama ujenzi wa nyumba n.k.
Picha
- Samora Machel Avenue ikiwa na N.I.C. House
- Feri ya kuvuka Kigamboni, huku nyumba za jiji zikionekana ng'ambo ya bandari asilia
Marejeo
Tazama pia
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.