![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/1/1f/Wikipedia-logo-v2-ja.svg/langsw-640px-Wikipedia-logo-v2-ja.svg.png&w=640&q=50)
Wikipedia ya Kijapani
From Wikipedia, the free encyclopedia
Wikipedia ya Kijapani (Kijapani: ウィキペディア日本語版 au Wikipedia Nihongo-ban|tafsiri "Wikipedia: Toleo la lugha ya Kijapan") ni toleo la kamusi elezo ya Wikipedia kwa lugha ya Kijapani. Na kwa tar. 25 Juni ya mwaka wa 2008, Wikipedia ya Kijapani imefikisha zaidi ya makala 500,000[1], na kuifanya iwe toleo la Wikipedia ya tano kwa ukubwa baada ya Kiingereza, Kijerumani, Kifaransa na Kipoland.
Wikipedia hii ilianzishwa mnamo mwezi wa Septemba ya mwaka wa 2002, na kunako mwezi wa Aprili katika mwaka wa 2006, ilifikisha makala 200,000 na kwa mwezi wa Juni katika mwaka wa 2008, ikafikisha makala 500,000. Hii ni Wikipedia kubwa kwa upande wa lugha ambazo si za Lugha za Ulaya, na ya pili kwa ukubwa ni ile Wikipedia ya Kichina.