![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/a/ae/Peter_Paul_Rubens_138.jpg/640px-Peter_Paul_Rubens_138.jpg&w=640&q=50)
Teresa wa Yesu
From Wikipedia, the free encyclopedia
Teresa wa Yesu (Avila, Hispania, 28 Machi 1515 - Alba de Tormes, Hispania, usiku wa kuamkia tarehe 15 Oktoba 1582) ni jina la kitawa la Teresa Sánchez de Cepeda Ávila y Ahumada, maarufu pia kama Teresa wa Avila.
![Mt. Teresa alivyochorwa na Pieter Paul Rubens](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/a/ae/Peter_Paul_Rubens_138.jpg/640px-Peter_Paul_Rubens_138.jpg)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/f/fa/Livio_Mehus_con_San_Pietro_d%E2%80%99Alcantara_che_comunica_santa_Teresa_d%E2%80%99Avila_%281683%29.jpg/320px-Livio_Mehus_con_San_Pietro_d%E2%80%99Alcantara_che_comunica_santa_Teresa_d%E2%80%99Avila_%281683%29.jpg)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/3/3e/Estasi_di_Santa_Teresa.jpg/640px-Estasi_di_Santa_Teresa.jpg)
Mwanamke halisi, bikira, utu wake ulikomaa: alikuwa na tabia ya kupendeza, uchangamfu na busara sana, uhodari na msimamo, uwezo wa kukubali hali iliyopo kwa kupanga vizuri na kufanikisha mambo.
Ni kati ya watu muhimu zaidi katika ya historia ya Kanisa ya karne ya 16, katika historia ya utawa na katika teolojia ya Kiroho kutokana na urekebisho aliouanzisha katika shirika la Wakarmeli (wanawake na wanaume vilevile) na kutokana na maandishi yake juu ya maisha ya kiroho yanayomfanya mwalimu wa sala aliye bora kuliko wote.
Alitangazwa na Papa Paulo V kuwa mwenye heri tarehe 24 Aprili 1614, na Papa Gregori XV kuwa mtakatifu tarehe 12 Machi 1622, na hatimaye na Papa Paulo VI kuwa mwalimu wa Kanisa tarehe 4 Oktoba 1970.