![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/a/a5/William_Blake_007.jpg/640px-William_Blake_007.jpg&w=640&q=50)
Shetani
From Wikipedia, the free encyclopedia
Shetani (kwa Kiebrania שָׂטָן Satan, kwa Kigiriki Σατανᾶς Satanâs, kwa Kilatini Sátanas) ni jina linalomaanisha "Mpinzani"; "Mshtaki".
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/a/a5/William_Blake_007.jpg/640px-William_Blake_007.jpg)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/9/9d/Paradise_Lost_12.jpg/640px-Paradise_Lost_12.jpg)
Shetani anajulikana pia kama Ibilisi (kutoka Kigiriki Diabolos, -ou, "Anayetenganisha"), Mtawala wa giza, Mkuu wa ulimwengu huu, Belzebub (jina la dhihaka kwa mungu Baal linalotafsiriwa "Bwana wa nzi"), Belial, Lusiferi (kutoka Kilatini Lucifer, "Mleta mwanga").
Kadiri ya imani ya dini mbalimbali, hasa zile zinazokubali ufunuo waliopewa Waisraeli, shetani ni malaika, roho, au mungu mdogo anayewakilisha uovu unaopingana na Mungu. Baadhi ya watu, kwa mfano Wakristadelfiani, hufundisha kwamba Shetani si nafsi hai, bali mfano tu wa uovu na dhambi.