![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/8/8c/Olav_der_Heilige07.jpg/640px-Olav_der_Heilige07.jpg&w=640&q=50)
Olaf II Haraldsson
From Wikipedia, the free encyclopedia
Olaf II Haraldsson (kwa Kinorwe asili: Ólafr Haraldsson; pia Olave; 995 – 29 Julai 1030) alikuwa mfalme wa Norway kuanzia mwaka 1015 hadi 1028.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/8/8c/Olav_der_Heilige07.jpg/640px-Olav_der_Heilige07.jpg)
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/7/70/Die_Alesunder_Kirche_ist_ein_beeindruckendes_Gesamtkunstwerk._01.jpg/640px-Die_Alesunder_Kirche_ist_ein_beeindruckendes_Gesamtkunstwerk._01.jpg)
Mtu wa watu, alieneza katika ufalme wake imani ya Kikristo aliyoifahamu huko Uingereza, akapambana na Upagani kwa bidii hadi alipouawa na maadui waliomshambulia kwa upanga huko Stiklestad[1].
Mwaka mmoja baadaye alitangazwa na askofu Grimketel huko Nidaros (Trondheim) kuwa mtakatifu. Jambo hilo lilichangia sana uenezi wa Ukristo nchini, naye akawa kiini cha utambulisho wa taifa[2][3].
Mwaka 1164 Papa Alexander III alithibitisha utakatifu wake.
Pamoja na Wakatoliki na Waorthodoksi[4], baadhi ya Walutheri na Waanglikana pia wanamheshimu hivyo.[5]