Upagani
From Wikipedia, the free encyclopedia
Upagani ni jina la kutaja imani za dini ambazo ama zinaabudu miungu mingi au ni dini za jadi.
Neno hili linatumiwa hasa na watu katika mapokeo ya Ukristo kutaja imani nyingine, lakini siku hizi, hasa katika nchi kadhaa za Ulaya, kuna pia vikundi vya watu ambao wanajiita hivi wenyewe.