Konrad wa Parzham
From Wikipedia, the free encyclopedia
Konrad wa Parzham O.F.M. Cap. ni jina la kitawa la Yohane Birndorfer (Bad Griesbach, Passau, Ufalme wa Bavaria, leo nchini Ujerumani, 1818 - Altötting, Bavaria, 1894) alikuwa bruda wa shirika la Ndugu Wadogo Wakapuchini na kufanya kwa unyenyekevu mkubwa kazi ya bawabu kwenye patakatifu pa Altötting kwa miaka 40 na zaidi.
Daima mkarimu kwa fukara, hakuacha mhitaji yeyote kuondoka bila kumpa kwanza maneno mazuri ya faraja ya Kikristo[1].
Alitangazwa na Papa Pius XI kuwa mwenye heri mwaka 1930 na mtakatifu mwaka 1934.