Sokwe mkubwa au sokwe peke yake ni jina la binadamu na nyani wakubwa wa familiaHominidae wanaofanana sana na binadamu. Tofauti na nyani wengine ni kuwepo kwa mkia; karibu nyani wote huwa na mkia lakini masokwe wakubwa hawana kabisa. Binadamu (Homo) anahesabiwa pia kama jenasi yenye spishi moja katika familia hii.
Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Masokwe wasiokuwa wanadamu wanaishi katika maeneo ya tropiki ya Afrika (masokwe mtu na ngagi) na Asia (orangutanu). Wote ni wakazi wa misitu ila tu masokwe mtu wanaoingia pia kwenye mbuga au savana. Wanadamu wanaishi duniani kote kwa kubadili mazingira yao, kuvaa nguo na kujenga majumba yanayowalinda kutoka joto kali ama baridi.
Ngagi Mashariki au Gorila Mashariki, Gorilla beringei (Eastern gorilla)
Ngagi-milima, Gorilla b. beringei (Mountain gorilla: Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Rwanda na Uganda)
Ngagi wa Uwanda wa Chini Mashariki, Gorilla b. graueri (Eastern lowland gorilla: Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo)
Ngagi Magharibi au Gorila Magharibi, Gorilla gorilla (Western gorilla)
Ngagi wa Nijeria, Gorilla g. diehli (Cross River gorilla: Nijeria na Kameruni)
Ngagi wa Uwanda wa Chini Magharibi, Gorilla g. gorilla (Western lowland gorilla: Kameruni, Jamhuri ya Afrika ya Kati, Gaboni, Ginekweta, Kongo, Jamhuri ya Demokrasia ya Kongo na Angola)
Makala hii kuhusu mnyama fulani bado ni mbegu. Je, unajua kitu kuhusu Sokwe (Hominidae) kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake? Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Wikiwand in your browser!
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.