![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/e/e8/Sant_Eusebio_di_Milano.jpg/640px-Sant_Eusebio_di_Milano.jpg&w=640&q=50)
Eusebi wa Milano
From Wikipedia, the free encyclopedia
Eusebi wa Milano (alifariki Milano, Italia Kaskazini, 8 Agosti 462) alikuwa askofu wa mji huo kuanzia mwaka 449.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/e/e8/Sant_Eusebio_di_Milano.jpg/640px-Sant_Eusebio_di_Milano.jpg)
Inasemekana alikuwa Mgiriki.
Alipigania imani sahihi na kujenga upya kanisa kuu lililobomolewa na Wahunni[1].
Papa Leo I alimuandikia barua (451).
Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.