Barua
From Wikipedia, the free encyclopedia
Barua ni ujumbe wa kimaandishi unaotumwa kwa mtu mwingine au watu wengine. Inawezekana kumwachia mtu ujumbe wa kimaandishi yaani barua mahali fulani lakini mara nyingi barua inatumwa kwa njia ya mtume au shirika linalofanya kazi hii kibiashara.
Kwa kawaida siku hizi barua inaandikwa kwenye karatasi ama kwa kalamu ama kwa taipureta ama kwa kutumia kompyuta na printa. Karatasi ya barua hukunjwa na kuwekwa ndani ya bahasha yenye jina na anwani ya mpokeaji juu yake. Siku hizi idadi kubwa ya ujumbe inaandikwa kwa njia ya baruapepe.