Ugiriki

nchi katika Ulaya Kusini-Mashariki From Wikipedia, the free encyclopedia

Ugiriki


Ugiriki (pia: Uyunani; kwa Kigiriki cha kisasa: Ελλάδα, Ellada, au Ελλάς, Ellas) ni nchi ya Ulaya Kusini-Mashariki iliyopo kusini mwa rasi ya Balkani.

Ukweli wa haraka
Ελληνική Δημοκρατία
Ellinikí Dimokratía

Demokrasia ya Ugiriki
Thumb Thumb
Bendera Nembo
Kaulimbiu ya taifa: Ελευθερία ή Θάνατος
(Eleftheria i thanatos - "Uhuru au mauti")
Wimbo wa taifa: Ύμνος εις την Ελευθερίαν - "Wimbo la Uhuru"
Thumb
Mji mkuu Athens
38°00 N 23°43 E
Mji mkubwa nchini Athens
Lugha rasmi Kigiriki
Serikali
Rais
Waziri Mkuu
Jamhuri
Katerina Sakellaropoulou (Κατερίνα Σακελλαροπούλου)
Kyriakos Mitsotakis (Κυριάκος Μητσοτάκης)
Uhuru
Ilitangazwa
Ilitambuliwa

25 Machi 1821
1829
Eneo
 - Jumla
 - Maji (%)
 
131,957 km² (ya 95)
1.51
Idadi ya watu
 - 2021 kadirio
 - 2012 sensa
 - Msongamano wa watu
 
10,678,632 (ya 85)
10,816,286
77/km² (ya 120)
Fedha Euro ()2 (EUR)
Saa za eneo
 - Kiangazi (DST)
EET (UTC+2)
EEST (UTC+3)
Intaneti TLD .gr 3
Kodi ya simu +30

-

1 Wananchi walikataza kurudi kwa ufalme tar. 8 Desemba 1974.
2 Prior to 2001: Greek Drachma.
Funga

Imepakana na Albania, Masedonia Kaskazini, Bulgaria na Uturuki. Upande wa kusini-magharibi na kusini-mashariki kuna pwani ndefu kwenye Bahari ya Mediteranea.

Jiografia

Kijiografia huwa na sehemu za Ugiriki bara, rasi ya Peloponesi upande wa kusini inayounganishwa kwa shingo ya nchi nyembamba, halafu visiwa vingi upande wa Bahari ya Aegean, Bahari ya Adria na kwenye Mediteranea yenyewe. Visiwa vikubwa zaidi ni Kreta, Euboea, Lesbo na Rhodos.

Historia

Thumb
Parthenon, katika Akropoli ya Athens, ni kielelezo cha Ugiriki wa Kale.

Ugiriki ni nchi yenye historia ndefu na maarufu sana, hata inaitwa "nchi mama ya Ulaya" na kitovu cha Ustaarabu wa magharibi, kwa sababu ndipo vilipoanza demokrasia, falsafa ya magharibi, fasihi ya magharibi, historiografia, sayansi ya siasa, tafiti za sayansi na hisabati, tamthilia na michezo ya Olimpiki.

Ugiriki ni nchi mwanachama wa Umoja wa Ulaya tangu 1981.

Watu

Lugha ya Kigiriki inaendelea kuandikwa kwa Alfabeti ya Kigiriki inayotumiwa tangu miaka 3000 iliyopita, lakini lugha yenyewe imebadilika. Wagiriki wa leo hawaelewi tena Kigiriki cha Kale moja kwa moja.

Wakazi wengi wanafuata dini ya Ukristo (93%), hasa katika Kanisa la Kiorthodoksi la Kigiriki (90%), halafu Waprotestanti na Wakatoliki. 2% ni Waislamu.

Tazama pia

Marejeo

Viungo vya nje


Maelezo zaidi Nchi za Umoja wa Ulaya ...
Funga
Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Ugiriki kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

Wikiwand in your browser!

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.

Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.

Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.