![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/7/75/St-aethelthryth.jpg/640px-St-aethelthryth.jpg&w=640&q=50)
Ethelreda wa Ely
From Wikipedia, the free encyclopedia
Ethelreda (pia: Ediltrudis, Editrudis, Audrey; jina asili: Æthelthryth au Æðelþryð au Æþelðryþe; Exning, Suffolk, 636 – Ely, Cambridgeshire, 23 Juni 679) alikuwa mwanamke wa ukoo tawala wa sehemu ya Uingereza aliyeolewa mara mbili na wafalme wa huko kwa sharti la kuachwa bikira.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/7/75/St-aethelthryth.jpg/640px-St-aethelthryth.jpg)
Hatimaye akawa mmonaki na abesi wa monasteri aliyoianzisha huko Ely, alipolea wanawake wengi kwa mfano wake na mashauri yake[1].
Kama dada zake wote wanne: Etelburga wa Faremoutiers, Vitburga wa Dereham, Seksiburga wa Ely na Setrida wa Faremoutiers anaheshimiwa tangu kale kama mtakatifu.
Sikukuu yake huadhimishwa na Wakatoliki, Waorthodoksi na Waanglikana tarehe ya kifo chake[2].