Afyuni
From Wikipedia, the free encyclopedia
Afyuni (kwa Kiarabu أفيون) ni dawa asilia inayopatikana kutokana na utomvu uliokauka wa maua ya mpopi (jina la kisayansi: Papaver somniferum - kwa Kiingereza: Opium poppy). Ndani yake mna kemikali mbalimbali ambazo ni kati ya dawa kali kabisa zenye uwezo wa kutuliza maumivu lakini zinasababisha pia ulevi unaozoesha watu haraka na kuwafanya wasiweze kuacha ulevi huo.