From Wikipedia, the free encyclopedia
Voyager 1 ni chombo cha angani kilichorushwa mwaka 1977 na shirika la NASA nchini Marekani kwa kusudi la kupeleleza anga-nje katika mfumo wa Jua letu hadi anga-nje kati ya nyota. Inaendelea kufanya kazi na kutuma data inayokusanya kwa kutumia vyombo vya upimaji ndani yake.
Voyager 1 ni chombo cha kutengenezwa na binadamu kilichofikia umbali mkubwa na Dunia yaani 145 vizio astronomia vinavyolingana na kilomita bilioni 21.6; nuru ya Jua inahitaji zadi ya masaa 20 kufikia Voyager 1 (hali ya Mei 2019).
Mwaka 2012 ilitembea nje ya mzingo wa Pluto katika kanda ya heliosferi penye mata ya mwisho inayoshikwa na graviti ya Jua ikiandaa kuondoka katika mfumo wa Jua letu kabisa na kuingia anga-nje kati ya nyota.
Voyager 1 ilipita karibu na sayari za Mshtarii na Zohali na kupiga picha za sayari hizi na miezi yao. Inaendelea kupima mnururisho uliopo angani na kutuma data duniani. Inachukua nguvu yake kutoka beteri zenye plutoni nururifu zinazozidi kufifia. Imekadiriwa kwamba kifaa cha mwisho kinachoweza kupima data kitazimika mwaka 2013.
Voyager 1 imeshapita katika Ukanda wa Kuiper ikieleka sasa kwenda wingu la Oort. Imeshapita eneo la heliosferi.
Voyager 1 inaendelea huko gizani na mwezi wa Mei 2019 ilifikia umbali wa km bilioni 21.6 au vizio astronomia (umbali kati ya Jua na Dunia) 145[1]. Bado inatuma data kuhusu uga sumaku ya Jua. Watafiti kutoka Ugiriki (Dialynas Kostas na wengine) walitumia data zake pamoja na Voyager 2 na Cassini kusema kumbe heliosferi ina umbo la tufe bila mkia mkubwa jinsi iliyoaminiwa awali.[2]
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.