Theodosi wa Kiev

From Wikipedia, the free encyclopedia

Theodosi wa Kiev

Theodosi wa Kiev au Theodosi Pekerski (kwa Kirusi Феодосий Печерский; kwa Kiukraina Феодосій Печерський; Vasylkiv, 1009 - Kiev, 3 Mei 1074) alikuwa mmonaki wa karne ya 11 aliyeleta umonaki wa kijumuia kadiri ya kanuni ya Theodori wa Studion katika sehemu za Kiev (leo nchini Ukraina) na pamoja na Antoni wa Kiev alianzisha monasteri maarufu ya Mapango ya Kiev.

Thumb
Picha takatifu ya Mt. Theodosi.

Alitangazwa na Kanisa la Kiorthodoksi la Urusi kuwa mtakatifu. Anaheshimiwa hivyo na Kanisa Katoliki pia.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 3 Mei[1][2] lakini pia tarehe 14 Agosti.

Tazama pia

Tanbihi

Viungo vya nje

Loading related searches...

Wikiwand - on

Seamless Wikipedia browsing. On steroids.