Tauni
From Wikipedia, the free encyclopedia
Tauni (au kipukusa; kwa Kiingereza: plague au pestilence) ni ugonjwa unaoambukiza watu wengi sana unaosababishwa na bakteria Yersinia pestis ya familia Enterobacteriaceae.


Inapatikana kwa kawaida katika maeneo kadhaa ya dunia yasiyo na maendeleo.[1]
Kadiri ya athira juu ya mapafu na hali nyingine za mgonjwa, inaweza kuenea kupitia hewa, kwa kugusana na kwa nadra kwa njia ya chakula kisichopikwa vya kutosha.
Dalili zinategemea ugonjwa umemshika mtu wapi zaidi: tezi, mishipa ya damu au mapafu.
Tiba ikiwahi inaweza kumponya mtu.
Historia
Zamani tauni iliua watu wengi: kwa miaka michache hata nusu ya Wachina wote, halafu theluthi ya Wazungu wote.
Biblia inazungumzia ugonjwa huo.
Barani Afrika ugonjwa ulienea mara kadhaa, lakini mtawanyiko wa watu katika maeneo makubwa haukuisaidia tauni kuwapata watu wengi zaidi kama kwenye msongamano mkubwa.
Ni maarufu juhudi za Wajerumani kukomesha tauni katika koloni lao la Afrika Mashariki ya Kijerumani mwishoni mwa karne ya 19 kwa kulipa kiasi kadhaa kwa kila mzoga wa panya, mnyama anayesambaza bakteria hizo kupitia viroboto wake.[2]
Tanbihi
Tazama Pia
Marejeo
Viungo vya nje
Wikiwand - on
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.