From Wikipedia, the free encyclopedia
Kaizer Chiefs ni klabu ya Afrika Kusini, iliyoanzishwa mnamo 7 Januari 1970 katika sehemu ya Soweto, mjini Johannesburg. Jina lingine la timu hii ni Amakhosi ambayo inamaanisha "mabwana" au "Chiefs" katika lugha ya Zulu. Wao kwa kawaida kucheza mechi zao za nyumbani katika viwanja wa FNB, ABSA au Ellis Park. . Hiki ndicho klabu kubwa zaidi nchini Afrika Kusini katika masuala ya mafanikio. Pia klabu hii ni yenye wafuasi wengi zaidi nchini Afrika Kusini na nchi jirani za Botswana, Zimbabwe, Zambia nk Inasemekana kwamba klabu hii ina zaidi ya wafuasi milioni 16.
Wao wana uelekezano wa kimitaa na Orlando Pirates, ni klabu ya Soweto ambayo mwanzilishi wa Chiefs, Kaizer Motaung aliichezea mapema katika wasifu wake.
Chiefs wamepigwa marufuku na Shirikisho la kandanda la Afrika (CAF) kutoshiriki katika mashindano ya klabu ya Afrika hadi mwaka wa 2009 baada ya kujiondoakutoka kwa kombe la Shirikisho la CAF mwaka wa 2005. Hii ni mara ya pili katika muda wa miaka minne kwamba Chiefs wameadhibiwa na CAF kwa kukataa kushiriki katika shindano hilo lililopangwa la CAF.
Kaiser Chiefs, bendi ya Uingereza inayocheza muziki wa Indie / britpop, ilipata jina lake kutoka kwa klabu kwa sababu Lucas Radebe, mchezaji wa zamani wa Kaizer Chiefs, alikuwa nahodha wa Leeds United, timu waliokuwa wakiishabikia.
Kaizer Chiefs ilianzishwa mwaka wa 1970 muda mfupi baada ya kurejea kwa Kaizer "Chincha Guluva" Motaung kutoka Marekani ambako alicheza kama mshambuliaji wa klabu ya Atlanta Chiefs ya Ligi ya Soka ya Amerika Kaskazini (NASL).
Watu wengine kadhaa wamecheza majukumu muhimu katika malezi na ukuaji wa Chiefs, pamoja na marehemu Gilbert Sekgabi, Clarence Mlokoti, China Ngema, na Ewert "The Lip" Nene.
Kaizer Chiefs –pia inajulikana kama Amakhosi na mashabiki wake-ilikuwa moja ya klabu za kwanza kugeuka kuwa klabu ya utaalamu kikamilifu. Makao yao makuu ni Kaizer Chiefs V illage, katika sehem ya Naturena, kilomita sita kusini ya Johannesburg.
Mbali na rekodi yake ya kuvutia ya mataji 80 katika miaka 36, Chiefs pia wameweka vigezo katika udhamini wa soka ya mitaa.
Msimu wa 2001/2002 ilikuwa moja ya misimu bora ya klabu hii, kwani lilishinda nyara nne kuu katika miezi minne. Nyara hizi zilijumuisha Vodacom Challenge, BP Top Eight, kombe la Coca-Cola, na kombe la CAF la mabingwa, pia inajulikana kama "kombe la Mandela."
Kwa kulishinda Kombe la Mandela, Chiefs walikwenda kucheza na mabingwa wa wakati huo wa ligi ya mabingwa ya CAF, Al-Ahly ya Misri katika kombe la Super. Mwezi Aprili 2002, mafanikio ya Kaizer Chiefs yalitambuliwa kwa kuchaguliwa kama "Klabu ya CAF ya Mwaka."
Katika msimu wa 2003/2004 Chiefs walipewa tuzo la Fair Play katika Kombe la Amani nchini Korea Kusini. Chiefs walikamilisha msimu kama mabingwa wa ligi kwa kushinda PSL kwa mara ya kwanza katika historia yao.
Katika msimu wa soka wa 2004/2005, Chiefs waliwapita viongozi wa muda mrefu wa ligi hiyo (Orlando Pirates) katika mechi ya mwisho ya msimu kutetea taji lao la PSL. Chini ya uongozi wa kocha mwenye asili ya Kiromania, Ted Dumitru, mshambuliaji wa Zambia, Collins Mbesuma, alikuwa na msimu wa kuvunja rekodi kwa kufunga mabao 35 katika mashindano yote.
Ushiriki wa Kaizer Chiefs katika mashindano ya Afrika ulisimamishwa na marufuku ya Shirikisho ya Kandanda ya Afrika (CAF). Hata hivyo, Kaizer Chiefs itarejea mashindanoni kombe la kila mwaka la Vodacom Challenge ambayo itajumuisha Kaizer Chief na Orlando Pirates pamoja na klabu ya Ulaya itakayoalikwa. Chiefs wameshinda kombe la Vodacom Challenge mara 4 tangu kuanzishwa kwake. Waliicharaza timu changa ya Manchester United mwaka wa 2006 na kushinda nyara hiyo.
Manmo Machi 2007, kocha Ernst Middendorp aliiacha klabu ya Chiefs. Mara moja klabu lilimwajiri kocha wa zamani wa Orlando Pirates Kostadin Papic kwa salio la msimu wa 2006/07.
Muhsin Ertugral alirudi msimu wa 2007/2008 kuanza hisabu yake ya pili na Chiefs kwa kuwa tayari ameikocha Glamour of Soweto Boys kuanzia mwaka wa 1999 hadi 2003.
Mechi kati ya Kaizer Chiefs na Orlando Pirates ni moja ya mechi zinazogombewa kwa nguvu na umakini katika ulimwengu wa kandanda, na ikilinganishwa na mechi zingine nyngi zinazochezwa katika ligi ya Afrika Kusini, mechi kati ya wapinzani hawa wawili kuvutia idadi kubwa ya wafuasi.
GP | W | D | L | NI | GA | |
---|---|---|---|---|---|---|
Chiefs | 34 | 12 | 12 | 10 | 32 | 30 |
Pirates | 34 | 10 | 12 | 12 | 30 | 32 |
Makipa
Madifenda
Wachezaji wa kiungo cha kati
|
Washambuliaji
|
1. Gert Schalkwyk 1
2. Jose Torrealba 0
Mchezaji wa Msimu: Siphiwe Tshabalala
Mchezaji wa Wachezaji wa Msimu: Siphiwe Tshabalala
Bao la Msimu: Siphiwe Tshabalala
Mchezaji mwenye mabao mengi: Siphiwe Tshabalala
Uamuzi wa wasomaji wa Amakhosi Magazine : Siphiwe Tshabalala
Mchezaji aliyevaa vizuri: Jimmy Tau
Tuzo la Fair Play: Arthur Zwane
Mchezaji aliyeboreka zaidi: Serge Djiehoua
Ni ukumbi wa nyumbani wa baadaye wa klabu ya Kaizer Chiefs. Kaizer Chiefs itakuwa timu ya kwanza ya kandanda nchini Afrika Kusini kuwa na uwanja wao wa kibinafsi wakati uwanja(Amakhosi) wa idadi ya viti 55000 utakapokamilika mnamo Aprili 2010. Amakhosi imetumia zaidi ya viwanja 9 mjini Johannesburg kama makao ya mechi zao za nyumbani. Uwanja mpya unatengenezwa kwa gharama ya randi bilioni 1.2 na itakuwa sehemu ya michezo mingi kwa jumla inayojengwa katika sehemu ambayo ni kilomita 40 magharibi mwa Johannesburg.
Uwanja wa Amakhosi utakuwa tayari manmo Aprili 2010, huku tata iliyosalia, inayojumuisha viwanja vya raga na kriketi, hoteli ya michezo na kituo cha ununuzi rejareja – itakayokuwa ikiuza vifaa vya michezo – itajengwa katika hatua ya baadaye.
Serikali ya Mkoa wa Gauteng itajenga miundombinu zingine karibu na uwanja kama vile barabara na reli.
Uwanja wa Amakhosi pia utakuwa makao ya Programu ya Maendeleo ya Vijana wa Kaizer Chief na wachezaji wachanga Chiefs wakianza kuishi hapo mnamo Juni 2010. Uwanja wa Amakhosi utakuwa na vyombo vya habari vya hali ya sanaa pamoja na chumba cha wanahabari kitachoweza kuwatosha zaidi ya waandishi wa habari mia moja. Pia itakuwa na na zaidi ya majumba maalum 195 na sehemu maalum za utazamaji kwa mashabiki wa Amakhosi wenye ulemavu.
Mipango ya uwanja ni pamoja na eneo la makazi ya magari 3000 na litajengwa vyombo maalum vya kupaki kwa ajili ya mabasi na teksi kuhakikisha kwamba msongamano wa magari ndani na nje ya eneo hili ni laini.
Watengenezaji wa uwanja wameweka muda kwa uwanja wa Amakhosi ambayo inapaswa kufungua milango yake kwa umma mnamo Juni 2010.
First National Bank Stadium (FNB Stadium au Soccer City ) ni uwanja lililoko mjini Johannesburg, nchini Afrika Kusini. Liko karibu na makao makuu ya Shirikisho la Kandanda la Afrika Kusini (SAFA House ) ambapo ofisi mbili za FIFA na Kamati ya Mtaa ya Kuandaa kombe la dunia la mwaka wa 2010 liko. [2]