Mwanaharakati wa kisiasa wa Uholanzi na Amerika na mwandishi From Wikipedia, the free encyclopedia
Ayaan Hirsi Ali (kwa Kisomali: Ayaan Xirsi Cali: Ayān Ḥirsī 'Alī; alizaliwa: Ayaan Hirsi Magan, huko Somalia, 13 Novemba 1969)[1] ni mwanaharakati wa haki za wanawake, mwandishi, msomi na mwanasiasa wa zamani raia wa Uholanzi na Marekani.[2][3]
Alipata usikivu wa kimataifa kwa kuwa mkosoaji wa Uislamu na mtetezi wa haki za wanawake wa Kiislamu, akipinga kwa nguvu ndoa za kulazimishwa, mauaji ya heshima, ndoa za utotoni na ukeketaji wa wanawake.[4][5]Alianzisha shirika la kulinda haki za wanawake liitwalo AHA Foundation. Ayaan Hirsi Ali hufanya kazi kwa ajili ya Hoover Institution na American Enterprise Institute.[6][7]
Mnamo mwaka 2003, Hirsi Ali alichaguliwa kuwa mwanachama wa baraza la wawakilishi la Uholanzi.
Baba yake Ayaan Hirsi Ali, Hirsi Magan Isse, alikuwa mwanachama muhimu wa Somali Salvation Democratic Front na kiongozi katika mapinduzi ya Somalia. Hata hivyo, muda mfupi baada ya kuzaliwa kwake, baba yake alifungwa gerezani kwa sababu ya kupinga serikali ya Kijamaa ya Siad Barre.
Baba yake Hirsi Ali alikuwa msomi na mpinzani wa serikali, pamoja na kuwa Muislamu mcha Mungu. Aliwahi kusoma nje ya nchi na alipinga vikali ukeketaji wa wanawake. Lakini wakati baba yake akiwa gerezani, bibi yake Hirsi Ali alimleta mwanaume kufanya ukeketaji huo akiwa na umri wa miaka mitano. Kwa bahati nzuri, bibi yake hakumpata mwanamke wa kufanya ukeketaji, kwani inasemekana kwamba unakuwa "mpole zaidi" ukifanywa na wanaume.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.