![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/e/e1/Drought.jpg/640px-Drought.jpg&w=640&q=50)
Ukame
From Wikipedia, the free encyclopedia
Ukame (kwa Kiingereza "Drought") ni hali ya hewa ya sehemu au mahali fulani inayofanya pakose maji ya kutosha kwa muda mrefu[1]. Kwa kawaida hii inamaanisha kipindi ambako kuna mvua kidogo, au kupungukiwa kwa usimbishaji mwingine kama theluji.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/e/e1/Drought.jpg/640px-Drought.jpg)
Ukame unatokea pia pale ambako watu na kilimo wanategemea maji kwa umwagiliaji na vyanzo vingine vya maji vinakauka.
Ukame unaweza kuhatarisha uhai wa mimea, wanyama na watu, ambao wote wanahitaji maji.