Ufalme wa Nkore
From Wikipedia, the free encyclopedia
Ufalme wa Nkore (kwa Runyankore; kwa Kiingereza: Ankole) ulikuwa himaya ya kitamaduni za Kibantu huko Uganda. Himaya hiyo ilikuwa inapatikana upande wa Kusini Magharibi mwa Uganda, Mashariki mwa Ziwa Edward. Himaya hiyo ilikuwa ikitawaliwa na serikali iliyojulikana kama vile Mugabe au Omugabe.
Watu wake walijulikana kama Banyankole (wakiwa wengi) na Munyankole (akiwa mmoja) hivyo lugha yao ya kibantu ilijulikana kama Runyankole.
Ufalme huo ulikubali ulinzi wa Uingereza tarehe 25 Oktoba 1901[1]. Ulifutwa rasmi mwaka 1967 chini ya utawala wa serikali ya rais Milton Obote na haujarudishwa rasmi.[2]