Ufalme wa Muungano
From Wikipedia, the free encyclopedia
Ufalme wa Muungano wa Britania na Eire ya Kaskazini (kwa Kiingereza: United Kingdom of Great Britain and Northern Ireland); kifupi: "Ufalme wa Muungano" (Kiing.: United Kingdom) ni nchi ya visiwani ya Ulaya ya kaskazini-magharibi. Mara nyingi huitwa kwa Kiswahili "Uingereza" tu ingawa nchi ya Uingereza ni moja tu kati ya sehemu za ufalme huo pamoja na Uskoti, Welisi na Eire ya Kaskazini.
| |||||
Kaulimbiu ya taifa: "Dieu et mon droit" (Kifaransa) "Mungu na haki yangu" | |||||
Wimbo wa taifa: "God Save the Queen" | |||||
Mji mkuu | London 51°30′ N 0°7′ W | ||||
Mji mkubwa nchini | London | ||||
Lugha rasmi | Kiingereza | ||||
Serikali 1: Mfalme Ufalme wa Muungano 2: Waziri Mkuu wa Ufalme wa Muungano |
bunge la ufalme wa kikatiba wa muungano 1: Charles III wa Uingereza 2: Rishi Sunak MP | ||||
' |
|||||
Eneo - Jumla - Maji (%) |
243,610 km² (80th) 1.34% | ||||
Idadi ya watu - 2019 kadirio - 2011 sensa - Msongamano wa watu |
67,545,757 (22nd) 63,181,775 270.7/km² (50th) | ||||
Fedha | Pound Sterling (£) (GDP ) | ||||
Saa za eneo - Kiangazi (DST) |
Greenwich Mean Time (GMT) (UTC+0) British Summer Time (BST) (UTC+1) | ||||
Intaneti TLD | .uk | ||||
Kodi ya simu | +44
- |
Katika karne zilizopita nchi iliongoza mapinduzi ya viwanda duniani, ilienea katika mabara yote kwa makoloni yake mengi ikabaki hadi leo kati ya nchi muhimu zaidi ulimwenguni.
Ni mwanachama mwanzilishi wa Umoja wa Mataifa, ambapo ana kiti cha kudumu na kura ya turufu katika Halmashauri ya Usalama.
Miaka 1974-2020 ilikuwa pia ni mwanachama wa Umoja wa Ulaya; ilijiondoa baada ya kura ya wananchi.