Charles III wa Uingereza
From Wikipedia, the free encyclopedia
Charles III (alizaliwa 14 Novemba 1948 kama Charles Philip Arthur George katika Buckingham Palace, London) ni mfalme wa Ufalme wa Muungano wa Britania na Eire ya Kaskazini tangu tarehe 8 Septemba 2022. Alipokea cheo hicho kutokana na kifo cha mama yake Malkia Elizabeth II[1].
Alirithi pia cheo cha ufalme wa nchi huru 14 zinazoitwa Commonwealth Realms:
- Antigua na Barbuda
- Australia
- Bahamas
- Belize
- Kanada
- Grenada
- Jamaika
- New Zealand
- Papua Guinea Mpya
- Saint Kitts na Nevis
- Saint Lucia
- Saint Vincent na Grenadini
- Visiwa vya Solomon
- Tuvalu
Yeye pia ni mkuu wa Jumuiya ya Madola, bwana wa maeneo yaliyopo chini ya Taji la Uingereza na mkuu wa kidunia wa Kanisa Anglikana nchini Uingereza.