Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa
From Wikipedia, the free encyclopedia
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ni mkono muhimu na wenye nguvu wa Umoja wa Mataifa. Baraza la Usalama linajadili masuala ya usalama na amani kati ya mataifa na kuwa na madaraka ya kutoa maazimio.
Baraza la Usalama lilikuwa na mkutano wake wa kwanza tarehe 17 Januari mwaka 1946 katika jumba la Church House mjini London. Tangu mkutano huo, baraza hilo ambalo halifungi mikutano yake, limesafiri kwa upana, likifanya mikutano katika miji mingi, kama vile Paris na Addis Ababa, ila kwa kawaida katika makao yake makuu katika jumba la Umoja wa Mataifa mjini New York.