![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/b/b3/Short-toed_Treecreeper_%2528Certhia_brachydactyla%2529cropped.jpg/640px-Short-toed_Treecreeper_%2528Certhia_brachydactyla%2529cropped.jpg&w=640&q=50)
Tambarazi
From Wikipedia, the free encyclopedia
Tambarazi ni ndege wadogo wa familia Certhiidae. Wana rangi ya kahawia au kijivu na madoa au michirizi nyeupe mgongoni na nyeupe chini. Domo lao limepindika na linatumika ili kutafuta wadudu chini ya gome. Tambarazi madoadoa ni spishi pekee ya Afrika kwa kweli. Inatokea Uhindi ya kaskazini pia. Huko Afrika ya Kaskazini kuna nususpishi ya tambarazi wa Ulaya: tambarazi kaskazi.
Maelezo zaidi Uainishaji wa kisayansi, Ngazi za chini ...
Tambarazi | ||||||||||||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
![]() Tambarazi madoadoa | ||||||||||||||
Uainishaji wa kisayansi | ||||||||||||||
| ||||||||||||||
Ngazi za chini | ||||||||||||||
Jenasi 2 na spishi 11:
| ||||||||||||||
Funga
Tambarazi hula wadudu tu. Tambarazi madoadoa hulijenga tago lao kwa umbo la kikombe juu ya tawi la mlalo na hulificha chini ya kuvumwani, mavi ya viwavi na tandabui. Spishi nyingine hulijenga tago lao kwa umbo la kikombe juu ya vijiti vilivyokwama kati ya gome na shina. Jike huyataga mayai 3-9.