Sayari kibete
From Wikipedia, the free encyclopedia
Sayari kibete (kwa Kiingereza dwarf planet) ni kiolwa cha angani kinachofanana na sayari ndogo lakini hakitimizi tabia zote za sayari kamili. Masi yake yanatosha kufikia umbo la tufe sawa na sayari kamili, lakini haikusafisha obiti yake kwa kujivutia sehemu kubwa sana za violwa vya angani vidogo vinavyozunguka kwenye obiti hiyohiyo.
Idadi ya sayari kibete haijulikani. Kufikia 2021, vitu 9 vinavyojulikana vinafikiriwa kuwa vibete, 8 kati yao katika obiti zaidi ya Neptuni.