From Wikipedia, the free encyclopedia
Maada (kutoka Kiarabu; pia: mata kutoka Kiingereza matter) ni neno pana linalojumlisha vyote vinavyoweza kuonekana, kusikika, kuguswa, kuchunguzwa n.k., ikiwemo hasa maada ya kawaida inayoundwa na atomi ambazo tena zinaundwa na kiini cha protoni na neutroni, kikizungukwa na wingu la elektroni.[1][2] Hivyo maada ni kitu chochote chenye uzito na kinachoweza kuchukua nafasi.
Tangu karne ya 20 ufafanuzi sahihi wa maada umeshindikana kutokana na maendeleo ya sayansi, nayo si tena jambo la msingi katika fizikia kama ilivyokuwa awali.[3][4]
Maada inapatikana kwa kawaida katika hali nne: mango, kiowevu, gesi na utegili. Maada huweza kubadilika pale tu halijoto inapobadilika. Badiliko la maada linaweza kuwa kutoka gesi kwenda yabisi mfano mvuke kuwa barafu, yabisi kwenda gesi mfano barafu kuwa mvuke, kimiminika kuwa yabisi mfano maji kuwa barafu n.k.
Hivyo matawi mbalimbali ya sayansi yanatumia neno maada kwa maana tofautitofauti.[5][6][7]
Falsafa pia inatumia neno hilo, hasa kwa kutofautisha maada na roho, na hivyo ulimwengu unaoonekana na ule ambao hauonekani, lakini unasadikika kuwepo.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.