![cover image](https://wikiwandv2-19431.kxcdn.com/_next/image?url=https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/b/b3/Shabbat_meal.jpg/640px-Shabbat_meal.jpg&w=640&q=50)
Sabato
From Wikipedia, the free encyclopedia
Sabato (kwa Kiebrania: שבת, shabbāt, yaani pumziko kwa Kiswahili) ni siku ya pumziko ya kila juma katika Uyahudi kwa ujumla na hasa katika nchi ya Israeli.
![Thumb image](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/b/b3/Shabbat_meal.jpg/640px-Shabbat_meal.jpg)
Desturi hiyo imesababisha simulizi la kitabu cha Mwanzo (1:1-2:4a) katika Biblia ya Kiebrania kuhusu jinsi Mwenyezi Mungu alivyomaliza kuumba mbingu na nchi kwa siku sita akaona vema kupumzika siku ya saba.
Wayahudi tangu kale wameona fahari kufuata mfano wa Mungu wakipumzika siku ya saba. Sabato husheherekewa kila Jumamosi kuanzia saa za jioni kwenye Ijumaa hadi jioni ya Jumamosi.
Kati yao, wale wanaofuata dini huanza kwa sala ya jioni kwenye sinagogi halafu kwa chakula cha pekee nyumbani.