From Wikipedia, the free encyclopedia
Mti wa Krismasi ni mti unaopambwa ili kuadhimisha Noeli (Krismasi).
Desturi hiyo ilianzia katika Ujerumani; kuna ushuhuda kutoka karne ya 15 kuhusu miti ya Krismasi, hasa kutoka sehemu za kusini-magharibi za Ujerumani. Hapo huitwa Weihnachtsbaum au Christbaum) [1][2]
Maana yake kiasili ni mti wa Paradiso. Katika kalenda ya kanisa tarehe 24 Desemba ilikuwa siku ya kukumbuka Adamu na Eva. Hivyo ilikuwa kawaida kuwa na maigizo kanisani yaliyosimulia habari za Biblia zinazotokea katika masomo ya liturgia ya Krismasi. Mti wa Paradiso unahusiana na masimulizi ya dhambi ya asili na ujumbe wa Kristo kama Mwokozi anayekuja kuondoa dhambi hiyo.
Kutoka maigizo ya kanisani ishara ya mti uliopambwa matunda na vyakula mbalimbali iliingia katika nyumba za Wakristo ambako ulipambwa zaidi kwa matunda, keki tamu na pipi kwa watoto. Umekuwa mapambo ya nyumbani kwa majira ya Krismasi.
Ilienea nje ya Ujerumani katika nusu ya pili ya karne ya 19, kwanza katika matabaka ya juu.[3]
Katika karne ya 18 ulianza kupambwa kwa mishumaa ambayo baadaye walibadilishwa na taa za umeme.
Siku hizi kuna mapambo ya aina nyingi kulingana na utamaduni wa mahali. Pengine juu ya mti unawekwa malaika kumwakilisha Malaika Gabrieli, au nyota kuwakilisha ile iliyongoza Mamajusi kutoka mashariki.
Papa Yohane Paulo II aliingiza desturi hiyo huko Vatikani mwaka 1982, ingawa kulikuwa na upinzani fulani.
Tangu Krismasi kuwa nafasi muhimu kwa uchumi kuna pia maduka mengi yanayoweka miti hii na katika mazingira ya kibiashara uhusiano wake na mti wa Paradiso umesahauliwa mara nyingi.
Katika mazingira ya Ulaya, ambako mti wa Krismasi ulibuniwa, sikukuu inatokea wakati wa majira ya baridi. Hapo miti karibu yote inapotewa na majani yao na kukauka. Ni miti ya aina ya misonobari pekee inayoendelea kuwa na majani na kupatikana kama miti mibichi wakati wa baridi. Kwa hiyo ni misonobari, misprusi hasa, iliyotumiwa tangu mwanzo kama miti ya Krismasi, mwanzoni msprusi wa Norwei lakini sikuhizi spishi nyingine pia.
Katika nchi kadhaa za Ulaya na Marekani misonobari hupandwa kwenye mashamba maalumu na kukatwa kabla ya Krismasi kwa matumizi ya majira ya Krismasi. Katika miaka ya nyuma desturi ya kuweka miti ya Krismasi kama mapambo kwenye nyumba, mitaa na maduka imeenea katika nchi nyingi hata pasipo Wakristo.
Siku hizi miti bandia ya Krismasi hutengenezwa kwa plastiki na kutumiwa hasa pasipo misonobari au pia katika mazingira ya mjini ambako misitu iko mbali. Miti bandia inaweza kupunguza hatari ya moto zinazotokea kila mwaka nyumbani wakati wa sikukuu.
Seamless Wikipedia browsing. On steroids.
Every time you click a link to Wikipedia, Wiktionary or Wikiquote in your browser's search results, it will show the modern Wikiwand interface.
Wikiwand extension is a five stars, simple, with minimum permission required to keep your browsing private, safe and transparent.